Mwnamuziki aliyewahi kuvunja rekodi ya
mwaka 2010 kwa kunyakua tuzo tano kwa mfululizo Abasi Kizasa" 20 pacent"
ameibuka na kutoa sababu za msingi za kushindwa kwenda kushiriki kwenye
mazishi ya mwanamuziki mwenzake Arbeth Mangwair kutokana na kuuguliwa
sana babaake mzazi ambae ana kansa ya utumbo.
Akiongea na Xdeejayaz 20 pacent alisema
kuwa " Siku wakati watu wanaondoka kwenda Morogoro kuzika huku mimi
babaangu alikuwa hali mbaya sana na alikuwa amelazwa Hospitalini hiyvo
isingekuwa rahisi kumuacha akiwa kwenye hali ile na mimi ndo nilikuwa
msimamizi wa kila kitu" Alisema mwanamuziki huyo.
Hata hivyo mwanamuziki huyo alimaliza
kusema kuwa kifo cha mwangwair ni pigo kubwa sana kwake kwa vile
walikuwa wanashirikiana mambo mengi sana kuhusu muziki na kujipanga
namna kukabiliana na maharamia wa muziki wanaotaka kuamudiwa kama Mungu
ili nyimbo zao zipigwe. Lakini licha ya hayo yote Mungu kampenda zaidi
Jina lake rihimidiwe Milele Amina.
No comments:
Post a Comment