Monday, 20 May 2013

KILICHO JIRI WAKATI NGASA ANASAINI MKATABA WA YANGA WA MIAKA MIWILI

Ngassa amezungumza kwa mara ya kwanza na kuthibitisha kwamba kweli amesaini Yanga.
“Ni kweli nimesaini Yanga, nisingeweza kuzungumzia suala hilo wakati nina mkataba ambao ulikuwa haujamalizika.
“Lakini baada ya mechi ya mwisho ya ligi, sasa niko huru kuanza kuutumikia mkataba wangu mpya,” alisema.
Mashabiki wa Yanga walimchukua Ngassa na kumvisha jezi ya njano na kijani, mara tu baada ya kumalizika kwa mechi kati ya Yanga na Simba kwenye Uwanja wa Taifa, jana.
Mashabiki hao walimvisha jezi hiyo na kumbeba na kumbeba na kuondoka naye hadi nje ya uwanja.
Azam FC ilimpeleka Simba kwa mkopo, lakini Simba imekuwa ikisema ilimuongezea mkataba wa mwaka mmoja na kumlipa Sh milioni 30 pamoja na gari.


Kama unahitaji picha ambazo alikuwa akisani mkataba huo mpya wa Yanga ingia hapa www.facebook.com/edwintanzania
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...