Monday, 13 May 2013

CHEK VIDEO NA PICHA, CLOUDS FM YAITIKISA DODOMA KATIKA UZINDUZI WA MSIMU MPYA WA RADIO HIYO


Katika kuzindua msimu mpya wa radio ya Clouds, ambao umefanyika ndani ya mji mkuu Dodoma, kwa siku tatu mfululizo, Clouds waliandaa semina kwa ajili ya kuwasaidia vijana, katika uelewa wa fursa zinazotuzunguka na kujituma kuhakikisha tunatumia fursa hizo kwa maendeleo yetu na taifa kwa ujumla.
Semina hiyo alifanyika katika ukumbi wa African dream hotel na kujumuisha vijana wa rika mbali mbali kutoka hapo pamoja na wasanii waliokuwepo kwa ajili ya shughuli hoyo
wasemaji wakuu siku hiyo walikuwa ni Mh Zitto Kabwe, mwanamuziki Mrisho Mpoto pamoja na bilionea mwenye umri mdogo 29 {kutokana na forbes}, Patrick Ngowi kutoka Arusha

Patrick Ngowi, mkurugenzi wa kampuni ya Helvetic Solar Contracators

Zenno Ngowi kutoka kampuni ya Tanzania Home Expo

mwanamuziki Mrisho Mpoto
Baada ya semina hiyo kufanyika, watu walielekea uwanja wa Jamhuri kwa ajili ya sherehe za uzinduzi huo ambapo wasanii mbali mbali walishiriki katika kutoa burudani kwa maelfu ya raia wa Dodoma waliofika uwanjani pale














No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...